Skip to main content

Featured

LATEST DEVELOPMENTS ON CARTOONIST OPPTERTUS FWEMA CASE.

  The case of Cartoonist Mr. Opptertus Fwema was scheduled for mention yesterday on 20th September 2022 before Aron Lyamuya  Resident Magistrate of kinondoni at kivukoni Courts. However, the Prosecution side submitted in court that they have no intention to proceed prosecuting the case. Hence, the prosecution entered nolle prosequi under section 91(1) of the Criminal Procedure Act. He was therefore discharged by the court in accordance to the law. However, after getting out of the court chambers, he was immediately arrested again and detained at the Oysterbay Police station for about two hours. His advocate (Shilinde Swedy) managed to obtain his bail and Mr. Fwema was later released after complying with bail requirements and requested to report at the police station again on Friday. Mr Fwema has not been charged with any offence after his rearrest. We encourage all artists to remain calm as his legal team maintains a close followup on this matter.

JE CINT IMESHAFANYA NINI?

 CREATIVE INDUSTRY NETWORK TANZANIA (CINT)  ni chombo kilichosajiliwa kihalali, chombo ambacho kinalenga kuwezesha mazingira bora katika tasnia ya Sanaa na Ubunifu, kwa  kufuatilia kwa ukaribu mambo ya Sera, Elimu Jinsia, Miundombinu, Uhuru wa kujieleza katika sanaa na mambo mengine yanayohusiana na haya.

Ni nia ya CINT kufanya kazi kwa ukaribu sana na  Taasisi mbalimbali, za Kiserikali na za Binafsi, Taasisi za haki za kijamii, wafadhili wa ndani na nje ya nchi, yote hii katika jitihada za kuwezesha wadau na washiriki wa tasnia za Sanaa na Ubunifu Tanzania kupata ufahamu utakaowezesha kazi za Tanzania kuwa na nafasi katika masoko ya duniani.  CINT ilianzishwa baada ya vikao kadhaa vya wadau wa sekta ambao waliona pengo la kukosekana kwa chombo kama hiki. Mpaka sasa  CINT ndio chombo chenye wanachama  wengi katika tasnia ya Ubunifu nchini.  CINT ina wanachama katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro, Iringa, Mwanza, Mbeya, Songwe, Dodoma na  Arusha. Kuanzia mwaka  2019, CINT imeweza kukutana na mamia ya wasanii na wadau wa sanaa na ubunifu katika mikoa mbalimbali Tanzania, kwa njia hiyo CINT imeweza kupata taarifa nyingi za hali ya sanaa na wasanii katika mikoa mbalimbali ya Tanzania. Tayari CINT ilikwisha toa jarida la ripoti yake ya kwanza ya mwaka 2019/20, ripoti hiyo iko katika lugha za KIswahili na Kiingereza na karibuni ripoti ya pili itatoka.

Jarada la ripoti ya mwaka 2019/20


Comments

Popular Posts